Jumanne, 14 Julai 2015

MASOMO YANAYOHARIBU ROHO YA MTU: (PART 3)

Chimbuko lingine la hatari ambalo twapaswa kujihadhari nalo siku zote ni kusoma vitabu vilivyotungwa na makafiri. Vitabu vya namna hiyo huandikwa kwa uongozi wa yule adui wa ukweli, na hakuna mtu awaye yote awezaye kuvisoma bila kuihatarisha roho. Kwa kweli wengine wanaoathirika na vitabu hivyo hatimaye huweza kupona; wote wanaojituliza kwa mvuto mbaya wa vitabu hivyo hujiweka ktk milki ya Shetani, naye huwafaidi sana. Wakiyakaribisha majaribu yake jinsi hiyo, hawana hekima ya kupambanua wala nguvu za kuyapinga. Kwa uwezo wa mivuto ya uzuri unaopoteza akili, kutoamini na ukafiri huimarika akilini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni