Jumanne, 14 Julai 2015

MASOMO YANAYOHARIBU ROHO YA MTU: (PART 2)

Katika mafundisho ya watoto na vijana, hekaya, hadithi za kizimwi, na hadithi za uongo sasa zimepewa nafasi kubwa. Vitabu vya namna hiyo hutumika shuleni, navyo hupatikana nyumbani mwa watu wengi. Wazazi ambao ni Wakristo huwezaje kuwaruhusu watoto wao kutumia vitabu vilivyojaa uongo jinsi hii? Watoto wakiuliza maana ya hadithi hizo ambazo ni kinyume cha mafundisho ya wazazi wao, hujibiwa kuwa hadithi hizo si za kweli; lakini hili halisaidii kuwaepusha na matokeo mabaya ya kuzitumia. Mawazo yatolewayo ktk vitabu hivyo huwapotosha watoto. Huingiza maoni ya uongo ya maisha na kuzaa pamoja na kuchochea tamaa ya mambo yasiyo ya hakika, yakuwaziwa tu. Kamwe vitabu vyenye kuipotosha kweli visiwekwe mikononi mwa watoto au vijana. Watoto wetu wanapojielimisha kwa njia hii, wasiruhusiwe kuwa na mawazo ambayo yatakuwa mbegu za dhambi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni