Jumapili, 19 Julai 2015

TABIA YA MBINGUNI HAINA BUDI KUPATIKANA DUNIANI:

Msidanganyike. Mungu hadhihakiwi. Utakatifu tu, wala si kitu kingine, ndio utakaowafanya kuwa tayari kwenda mbinguni. Unyofu na uchaji wa hakika ktk mambo ya maisha peke yake ndio uwezo wa kuwapa tabia safi, na bora, na kuwawezesha kuingia mbele za Mungu akaaye penye nuru isiyoweza kukaribiwa. Tabia ya mbinguni haina budi kupatikana hapa duniani, ama sivyo kamwe haipatikani tena. Basi, anza mara moja. Usidanganyike kuwa utafika wakati uwezapo kujitahidi kwa urahisi kuliko sasa. Kila siku huzidisha umbali wako kutoka kwa Mungu. Jitayarishe kwa ajili ya uzima wa milele. Zoeza mawazo ya moyo wako kuipenda Biblia, kupenda mikutano ya maombi, kupenda saa ya kumtafakari Mungu, na, zaidi ya yote, saa ambayo roho hushirikiana na Mungu. Uwe mwenye kufikiri mambo ya mbinguni ukipenda kuungana, na lile kundi la waimbaji wa mbinguni ktk makao ya juu.

Jumanne, 14 Julai 2015

MASOMO YANAYOHARIBU ROHO YA MTU: (PART 3)

Chimbuko lingine la hatari ambalo twapaswa kujihadhari nalo siku zote ni kusoma vitabu vilivyotungwa na makafiri. Vitabu vya namna hiyo huandikwa kwa uongozi wa yule adui wa ukweli, na hakuna mtu awaye yote awezaye kuvisoma bila kuihatarisha roho. Kwa kweli wengine wanaoathirika na vitabu hivyo hatimaye huweza kupona; wote wanaojituliza kwa mvuto mbaya wa vitabu hivyo hujiweka ktk milki ya Shetani, naye huwafaidi sana. Wakiyakaribisha majaribu yake jinsi hiyo, hawana hekima ya kupambanua wala nguvu za kuyapinga. Kwa uwezo wa mivuto ya uzuri unaopoteza akili, kutoamini na ukafiri huimarika akilini.

MASOMO YANAYOHARIBU ROHO YA MTU: (PART 2)

Katika mafundisho ya watoto na vijana, hekaya, hadithi za kizimwi, na hadithi za uongo sasa zimepewa nafasi kubwa. Vitabu vya namna hiyo hutumika shuleni, navyo hupatikana nyumbani mwa watu wengi. Wazazi ambao ni Wakristo huwezaje kuwaruhusu watoto wao kutumia vitabu vilivyojaa uongo jinsi hii? Watoto wakiuliza maana ya hadithi hizo ambazo ni kinyume cha mafundisho ya wazazi wao, hujibiwa kuwa hadithi hizo si za kweli; lakini hili halisaidii kuwaepusha na matokeo mabaya ya kuzitumia. Mawazo yatolewayo ktk vitabu hivyo huwapotosha watoto. Huingiza maoni ya uongo ya maisha na kuzaa pamoja na kuchochea tamaa ya mambo yasiyo ya hakika, yakuwaziwa tu. Kamwe vitabu vyenye kuipotosha kweli visiwekwe mikononi mwa watoto au vijana. Watoto wetu wanapojielimisha kwa njia hii, wasiruhusiwe kuwa na mawazo ambayo yatakuwa mbegu za dhambi.

MASOMO YANAYOHARIBU ROHO YA MTU:

Kwa ajili ya wingi wa vitabu na magazeti vinavyomiminika daima kutoka ktk mitambo ya kuchapisha, wazee kwa vijana hufanya mazoea ya kusoma haraka-haraka na kwa juu juu tu, na hivyo ubongo hupoteza uwezo wake wa kupokea mawazo yaliyounganika na yenye nguvu. Juu ya hayo, sehemu kubwa ya magazeti na vitabu ambavyo, kama vyura wa Misri, vinatapakaa nchini, sio kwamba nivya hali ya chini tu, visivyofaa, na vyenye kudhoofisha, bali ni vichafu na vyenye kuaibisha. Matokeo yake siyo kulevya na kuharibu akili tu, bali kuchafua na kuangamiza roho.

Jumatano, 1 Julai 2015

A TRUE KNOWLEDGE OF GOD:

Like our Saviour, we are in this in this world to do service for God. We are here to become like God in character, and by a life of service to reveal Him to the world. In order to be co-workers with God, in order to become like Him and reveal His character, we must know Him aright. We must know Him as He reveals Himself. A knowledge of God is the foundation of all true education and and of all true sevice. It is the only real safeguard against temptation. It is this alone that can make us like God in character. This is the knowledge needed by all who are working for the uplifting of their fellow men. Transformation of character, purity of life, efficiency in service, adherence to correct principles, all depend upon a right knowledge of God. This knowledge is the assential preparation both for this life and for the life to come. "The knowledge of the Holy is understanding." Proverbs 9:10.

Alhamisi, 18 Juni 2015

UPONYAJI WA MUNGU KUPITIA MAOMBI:

Kristo ni tabibu yule yule mwenye huruma sasa kama alivyokuwa wakati wa kazi zake hapa duniani. Ndani yake kuna zeri iponyayo kwa kila udhaifu wa mwili. Wanafunzi wake wa siku hizi wanatakiwa kuwaombea wagonjwa kama vile wanafunzi wa zamani wakivyowaombea. Uponyaji utafuata; kwakuwa kule kuomba kwa imani kutamuokoa mgonjwa yule" (Yakobo 5:14-15). Alipokuwa hapa duniani, Yesu alifundisha ya kwamba imani ni sehemu muhimu ya uponyaji wake. Yule mwanamke alipogusa upindo wa vazi lake Kristo na kupona ugonjwa wake, Kristo alimwambia,"Imani yako imekuponya." (Math 9:22). Wote wanaweza kupata imani ya Yesu na uweza wa Roho Mtakatifu. Tunayo nguvu ya Roho Mtakatifu , ahadi tulivu ya imani ambayo inaweza kudai ahadi zake Mungu. Niwajibu wetu kuwakabidhi kwa Mungu wagonjwa na wale wanaoteseka kwa njia ya mikono ya imani yetu.

Jumanne, 16 Juni 2015

UHUSIANO WETU NA SHERIA ZA MBINGUNI:

Sheria kuu zile zile zinazoongoza nyota na chembe ndogo sana (atom) huongoza pia maisha ya kibinadamu. Chanzo cha uhai wote ni Mungu. Kuivunja sheria yake, kimaumbile, kiakili, ama kimaadili, ni kujiweka mwenyewe kinyume na taratibu za Mungu ktk uumbaji wake wote, matokeo yake ni mafarakano, machafuko, na maangamizi. Juu ya viumbe vyake Mungu umewekwa wajibu mtakatifu wa: (1)Kutambua kwamba Mungu ndiye mwanzilishi wa sheria zote. (2)Kujifunza kuzielewa sheria za Mungu. (3)Kuzitumia sheria za Mungu ktk shughuli za kila siku za maisha yetu.

IMANI KTK UWEZA WA MUNGU:

Yatupasa kushirikiana na Mungu ktk kuitunza miili yetu. Upendo kwa Mungu ni wamuhimu kwa uzima na afya yetu, ili kuwa na afya kamili, mioyo yetu haina budi kujazwa na upendo na tumaini na furaha ktk Bwana. Afya bora kuliko kuliko zote ya mwili, akili, na roho inaweza kupatikana tu kwa kuunganishwa na nguvu za Mungu. Kadiri afya kijumla inavyozidi kuwa bora, ndivyo uwezo wetu wa kumheshimu na kumtukuza muumbaji na mkombozi wa wanadamu utakavyozidi kuwa mkubwa zaidi kwa njia ya kuakisi tabia yake kwa ulimwengu huu. Muungano kati ya ubinadamu na uungu hutokea ktk sehemu ya mbele ya ubongo. Neva za ubongoni zinazowasiliana na mfumo mzima wa mwili ndiyo njia pekee ya mbingu ya kuweza kuwasiliana na mwanadamu na kuyabadilisha maisha yake ya ndani. Uweza wa Mungu unapoungana na maisha ya kibinadamu, unaathiri; (1)Uhusiano wetu na Mungu. (2)Uhusiano wetu na sheria za mbinguni.(3)Huduma yetu kwa Mungu. (4)Huduma yetu kwa wengine.

Jumapili, 7 Juni 2015

REVIVAL & REFORMATION:

There is a science of Christianity to be mastered a science as much deeper, broader, higher than any human science as the heavens are higher than the earth. The mind is to be disciplined, educated, trained; for we are to do service for God in ways that are not in harmony with inborn inclination. Hereditary and cultivated tendencies to evil must be overcome. Often the education and training of a lifetime must be discarded, that one may become a leaner in the school of Christ. Our hearts must be educated to become steadfast in God. we are to form habits of thought that will enable us to resist temtation. We must lean to look upward. The principles of the word of God princples that are as high as heaven, and that compass eternity we are to understand in their bearing upon our daily life. Every act, every word, every thought, is to be in accord with these principles. All must be brought into harmony with, and subject to, CHRIST.

Ijumaa, 5 Juni 2015

ADAMU WAWILI WAKUTANA:

Waliokombolewa walipokaribishwa ktk mji wa Mungu, kulikuwa na shangwe kuu. Adamu wawili karibu wakutana. Mwana wa Mungu atampokea baba wa taifa la kibinadamu, ambaye alimwumba,akatenda dhambi ambazo zilisababisha kusukubishwa kwa Mwokozi, na kupata akama ktk mwili wake. Adamu anapoona alama za misumari ktk mikono yake, anajitupa chini ya miguu ya Kristo. Mwokozi anamwinua na kumwambia atazame tena bustani ya Edeni, ambayo alifukuzwa kwa siku nyingi. Maisha ya Adamu yamekuwa ya huzuni nyingi. Kila mara alipoona majani yakinyauka na alipoua mnyama wa sadaka, iki ktmpatanisha na Mungu, yote hayo yalimktmbusha ubaya wa dhambi. Aliona uchungu wa ajabu, mambo hayo yote yakitupwa kwake, kwamba niyeye aliyesababisha, alijuta kabisa. Akafa ktk tumaini. Na sasa kwakuwa akisamehewa, amerudishiwa hali yake ya kwanza. Akijaa furaha tele, aliuona mti wa uzima uliokuwa chakula chake. Mwokozi anamwongoya kwenda kwemye mti wa uzima na akaambiwa ale matunda yake. Adamu aliona maeldu ya ukoo wake ambao wamekombolewa.

Alhamisi, 4 Juni 2015

SABBATH GATHERINGS

Sabbath day is the day that God planned for all human beings to get together to worship Him, the Creator and Redeemer of all mankind. This great day was set aside by the devine Creator to be used for His glory. Doing good works on the sabbath day is one of the best acts of keeping the sabbath holy. The sabbath belongs to God, and Jesus is Lord even of the Sabbath day. The Bible also says, All things were made through Him (JESUS) and without Him nothing was made that was made.

Jumatatu, 1 Juni 2015

MAKAO YAKO KTK YERUSALEMU MPYA.

Kamwe ulimwengu haujapata kuona mji kama huu, usio na wahalifu, mabanda ya maskini, wala polisi. Mji huu unatajwa kuwa ni "mke wa Mwana Kondoo" na nimakao mazuri ya wale wanaomfuata mwana kondoo popote aendapo. Ni mji wa kweli na halisi, unaokaliwa na watu halisi. Utakuwa ni kutimiza tumaini ka Ibrahimu."Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu." Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. Kwahiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao, maana amewatengenezea mji" Ebr 11:10,16. Hakuna mojawapo ya miji ya ulimwengu huu ulio na msingi halisi, kwasababu yote itapita kama ilivyopita miji ya nyakati za Ibrahimu.

NO TIME TO LOSE.

We have no time to lose. We know not how soon our probation may close. At the longest, we have but a brief lifetime here, and we know not how soon the arrow of death may strike our hearts. We know not how soon we may be called to give up the world and all its interests. Eternity stretches before us. The curtain is about to be lifted. But a few short years, and for everyone now numbered with the living the mandate will go forth.

Bible Principles of cure

For those who would regain or preserve health there is a lesson in the words of Scripture,"Be not drunk with wine, wherein is excess, but be filled with the Spirit."Ephesians 5:18.